
Jua Haki Zako
RFI Kiswahili · France Médias Monde
Show overview
Jua Haki Zako launched in 2025 and has put out 27 episodes in the time since. That works out to roughly 5 hours of audio in total. Releases follow a weekly cadence.
Episodes typically run under ten minutes — most land between 10 min and 10 min — and the run-time is fairly consistent across the catalogue. None of the episodes are flagged explicit by the publisher. It is catalogued as a SW-language Government & Organizations show.
The show is actively publishing — the most recent episode landed 3 days ago, with 16 episodes already out so far this year. Published by France Médias Monde.
From the publisher
Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Latest Episodes
View all 27 episodesKenya : Uhuru wa wanahabari si mjadala
Rueben Kigame na harakati zake kupigia haki
Unyanyasaji na kunyimwa haki kwa wanawake katika biashara za kimataifa
Kenya : Mchango wa masharika ya kiraia kwa jamii
Katika makala haya tunajikita kuangazia mchango wa mashariki yasiokuwa ya kiserikali kwenye jamii zetu. Tunaliangazia shirika la Corps Africa ambalo kwa ushirikiano jamii mbali mbali nchini Kenya limeendelea kuleta mageuzi kwa raia. Ili jamii kuendelea na kujitegemea inahitaji watu wa kufanikisha baadhi ya maswala kwa jamii kuja na mbinu ya namna gani ya kuwezesha jamii kujiendeleza. Kutokana na hili ndipo Corps Africa nchini Kenya huwatumia vijana kwa kuwatuma katika jamii mabalimbali, ili kusema na hizo jamii na kutambua namna gani au wanahitaji msaada gani.
Kenya: Pesa za majanga haziwafikii waathiriwa
Katika makala haya tunaangazia ripoti kuhusu ufadhili wa majanga na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo kame, iliochapishwa na masharika kadhaa likiwemo lile la Oxfarm. shaba ikilenga taifa la Kenya, Ripoti hii inaonyesha kuwa licha ya maeneo haya kuathirika zaidi na ukame, mafuriko na mabadiliko ya tabianchi, bado fedha nyingi hazifiki moja kwa moja kwa wananchi wanaohitaji msaada huo zaidi. Ripoti hiyo ya Oxafarm inaonyesha kuwa mfumo wa ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi nchini Kenya bado una changamoto nyingi, ikiwemo ukosefu wa uwazi, ushirikishwaji mdogo wa jamii, na utegemezi mkubwa wa fedha kutoka nje masharika ya nje
Kenya : Haki za wafanyibiashara wa soko la Kigomba
Katika makala haya tunaangazia haki za wafanyibiashara katika soko la Gikomba nchini Kenya. Kwa muda wafanyibiashara hao wamekuwa wakizozana na serikali kuhusu kipande cha ardhi cha soko hiyo. Skiza makala haya kufamu mengi zaidi.
Kenya : Haki za watoto wa kurandaranda mitaani
Kila mtotto ana haki kwa mjibu wa katiba za kila nchi na maazio ya kimataifa. Katika makala haya tunaanhazia haki za watoto wa kurandaranda mitaani. Skiza makala haya kufahamu mengi.
EAC : Wanawake wasilia nyuma katika harakati za amani
Kila Machi nane dunia, huadimisha siku ya kimataifa ya wanawake, katika makala haya tunaangazia sababu ambazo zimechangia wanawake kuachwa nyuma katika harakati za kutafuta amani. Skiza makala haya kufahamu mengi.
Haki za wakimbizi wanapokimbilia mataifa ya kigeni
Je ni masaibu gani wanayopitia wakimbizi wakati wanapokimbia nchi zao? Skiza makala haya kufahamu mengi.
Kenya: Mchakato wa kutoa taarifa za rushwa kwa tume ya EACC
Nchini Kenya tume ya kupambana na rushwa EACC imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mali ya umma haiporwi. Ila ni mchakato upi mtu anastahili kufuata kutoa taarifa kwa tume. Benson Wakoli alikiti chini Kipsang Sambae afisa wa EACC, tawi la Nakuru kufahamu mchakato wa kutoa taarifa kwa EACC.
Haki ya kuhifadhi taarifa za Siri
Je unafahamu kuhusu haki ya taarifa zako za siri kuhifadhiwa? na je unatambua hatua unazostahili kufuata iwapo zitatolewa? .
Human Right Watch : Haki zinakandamizwa pembe ya Africa
Makala haya yanaangazia ripoti ya Human Rights Watch iliyochapishwa tarehe 4 Februari 2026, inayozungumzia hali ya kutisha ya haki za binadamu katika eneo la Pembe ya Africa. Ripoti hiyo inaonyesha kuwa raia wa Sudan, Sudan Kusini na Ethiopia ndio wanaobeba mzigo mkubwa wa vita vya silaha vinavyoendeshwa kwa ukatili, ambapo pande zinazopigana mara nyingi hulenga raia kimakusudi. Human Rights Watch inasema mashambulizi haya dhidi ya raia yamekuwa jambo la kawaida, huku wahusika wakikosa kuwajibishwa. Kufahamu mengi skiza makala haya.
Kenya: Hatua za kutafuta haki kwa dhulma za kinadada mtaani Mathare
Kwa miaka mingi Beatrice Karole amekuwa akijitolea kuhamasisha jamii kuhusiana na hatua za kuchukua wakati wanapokabiliana na unyanyasaji wa jinsia. Akiwa na shirika la kinamama la Wanawake Mashinani Initiative katika eneo la Mathare Jijini Nairobi, amefanikiwa kuwaokoa jumla ya wanawake na watoto 30 katika mwaka 2025 ambao anajivunia kuwa licha ya kunyanyaswa, walipata haki yao.
Kenya: Wakulima wadogowadogo washinda kesi ya Sheria ya Mbegu na Mimea dhidi ya KEPHIS
Nchini Kenya, Sheria ya Mbegu na Mimea (The Kenya Seed and Plants Varieties Act), ambayo ilitishia kuwatoza faini na kuwafunga jela wakulima wadogo kwa kugawana mbegu ambazo hazijaidhinishwa, iliamuliwa kuwa kinyume cha katiba. Mahakama ya Kikatiba katika kaunti ya Machakos nchini Kenya ilitoa uamuzi wa kihistoria Novemba 27 2025 kuhusu uhalali wa Sheria ya Mbegu na Aina za Mimea. George Ajowi amekuwa akifuatilia kesi hii na kuandaa taarifa ifuatayo.
EAC : Dhuluma za kijinsia bado ni changamato kote duniani
Makala haya yanaangazia namana gani dhuluma za kijinsia zinaweza kabiliwa. skiza kufahamu mengi zaidi.
Kenya : Biashara ya ngono miongoni mwa vijana ni donda sugu
Juhudi za pamoja zinaendelezwa ili kukomesha biashara haramu ya wototo pwani ya Kenya. Kufahamu mengi zaidi skiza makala haya.
Kenya : Ahadi ya serikali kwa jamii za wachache
Kila disemba 18 dunia huadimisha siku ya Kimataifa ya Jamii za Walio Wachache siku inayolenga kuzikumbusha serikali na jamii wajibu wa kulinda haki, heshima na ushirikishi wa makundi ambayo kwa miaka mingi yamekuwa yakidai kuachwa nje mipango ya serikali Nchini Kenya, jamii za walio wachache, zikiwemo jamii za wafugaji wanaohamahama, zimekuwa zikidai hazitambuliwi kikamilifu, kukosa huduma za msingi, na kutengwa katika maamuzi muhimu ya kitaifa. Makala haya yanaangazia mipango ya serikali ya Kenya kwa jamii hizo.
Mpango wa kidijitali uliokwama unavyowanyima wanafunzi elimu ya kisasa Kenya
Mwaka 2016, Serikali ya Kenya ilizindua Mpango wa Mafunzo kwa Njia ya Kidijitali (DLP), ikiahidi kubadilisha elimu ya msingi ya umma kupitia teknolojia. Awamu ya kwanza ikigharimu walipa kodi zaidi ya Shilingi bilioni 30, huku kukiwa na mpango wa kupanua mradi huo kwa makadirio ya Shilingi bilioni 64. Takribani miaka kumi baadaye, mpango huo unazidi kukabiliwa na matatizo makubwa na hatimaye kukwama hivyo kuwanyima wanafunzi wa shule za msingi haki zao za kupata elimu ya kidijitali.Sikiliza
Kenya : Haki ya wafanyakazi nje ya nchi
Katika Juhudi za raia wa Africa Kutafuta ajira nje ya nchi wengine wamejipata katika njia panda. Lakini ubalozi wa Austria nchini Kenya, unasisitiza taifa hilo ni salama kwa wafanyakazi wa kigeni. Skiza makala haya.
EAC : Haki ya matumizi ya mitandao
Je unafahamu haki zako wakati unatumia mitandao? na Je unafahamu kwamba haustahili kuvuka kiwango fulani wakati unatumia mitandao? Paul Brain ni mtaalamu wa matumizi ya mitandao anafanunua masharti ya matumizi ya mitandao.